• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Miji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Usafi na Mazingira
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Utoaji wa Leseni ya Biashara
    • Utoaji wa Leseni za Vileo
    • Utoaji wa Kibali cha Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Maagizo ya DC Twange kwa Watumishi wa Umma na Wafanyabiashara kuhusiana na utoaji wa risiti za EFD

Imechapishwa: December 2nd, 2022

Na Nyeneu, P. R

Mkuu wa Wilaya ya Babati Mheshimiwa Lazaro Jacob Twange amewaagiza Maafisa Biashara na Maafisa wote wanaohusika wakasimamie zoezi la Matumizi ya Mashine za EFD katika utoaji wa risiti. DC Twange ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Kodi, ametoa maagizo hayo katika kikao cha Baraza la Biashara la Wilaya ambacho kilifanyika Disemba 2, 2022 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji wa Babati. Mhe. Twange amesema pia, Wilaya ya Babati haifanyi vizuri kwenye zoezi la utoaji wa risiti kwa mfanyabiashara na kudai risiti kwa mnunuzi. Hatua na adhabu kali zitachukuliwa kwa mfanyabiashara ambaye hata toa risiti na vilevile kwa mnunuzi ambaye hatadai risiti.

Pia Mhe. DC ameongeza kwa kuwaasa watumishi wa umma kuwa mstari wa mbele katika kudai risiti pale wanaponunua kwani watumishi wa umma ndio wanufaika wa kwanza na fedha zinazotokana na kodi kupitia mishahara. "Na sisi watumishi tunajijua, hatudai risiti sisi watumishi. Kwahiyo mtazamo ukibadilika kuanzia kwa sisi watumishi wa umma tunaolipwa mishahara inayotokana na kodi, tunatakiwa tuwe mstari wa mbele kudai risiti." alisisitiza Mkuu wa Wilaya. Mhe. Mkuu wa Wilaya amesema, kwa mtu yeyote atakayekamatwa kwa kosa la kutokutoa risiti au kutokudai risiti, hatokuwa mgeni wake kwa kuwa utaritibu unajulikana na unatakiwa ufuatwe bila kushurutishwa. "Naomba niseme wazi hapa, atakaye kamatwa na atakaye adhibiwa kwa kosa hili, huyu mimi sio mgeni wangu." Aliendelea kusisitiza Mhe. DC.

Mwisho, DC Twange ametoa rai kwa Wafanyabiashara kuwa watii maagizo haya ili wasiipoteze faida inayopatikana na biashara zao katika kulipia adhabu ambayo pengine imesababishwa na uzembe. "Kwahiyo wafanyabiashara kaeni vizuri, maana adhabu yenu ndo kubwa. Na mimi sioni sababu kwenye faida yako usishangae unatoa milioni tatu, milioni Nne na nusu bila utaratibu. Fedha inapatikana kwa mikakati na faida inayopatikana inatakiwa itumike kukuza mtaji wako au kuwekeza zaidi, sasa ukiwa tayari kuipoteza kwenye adhabu ambayo umeifanya kwa udhembe... sisi hatutakuwa sehemu ya kukusaidia kutatua hiyo changamoto. Pambaneni mtii sheria, toeni risiti pale mnapouza na wananchi wadai risiti wanapotoa hela zao kununua."


Picha zote na Nyeneu, P. R

Matangazo

  • Tangazo kwa waliopimiwa na kurasimishiwa viwanja - Sawe na Nangara December 25, 2022
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza - 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU November 09, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI NGAZI YA TATU July 27, 2022
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Miaka Miwili ya Rais Samia Manyara ni Shangwe tupu

    March 18, 2023
  • Waziri Kairuki atoa angalizo utekelezaji mradi wa BOOST

    December 13, 2022
  • Mhe. Jenista Mhagama awasisitiza watendaji wa ofisi yake kuwa na kauli nzuri na kutoa huduma bora kwa wananchi na watumishi wanaowahudumia

    December 04, 2022
  • Maagizo ya DC Twange kwa Watumishi wa Umma na Wafanyabiashara kuhusiana na utoaji wa risiti za EFD

    December 02, 2022
  • Tazama zaidi

Video

Halmashauri ya Mji wa Babati kuelekea miaka 61 ya Uhuru
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati