• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Miji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Usafi na Mazingira
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Utoaji wa Leseni ya Biashara
    • Utoaji wa Leseni za Vileo
    • Utoaji wa Kibali cha Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Idara ya Mifugo na Uvuvi

Bi.Rena Urio

Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi

IDARA YA MIFUGO NA UVUVI

1.0.    Utangulizi

Sekta ya Mifugo ina nafasi kubwa katika kujenga uchumi imara wa Taifa, kuongeza kipato kwa watanzania wanaotegemea mifugo na kutoa fursa ya ajira na kuhifadhi rasilimali za Taifa. Hii ni kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Mifugo ya mwaka 2006. Dira ya sekta ya Mifugo kama ilivyokubaliwa na wadau wa sekta mwezi Aprili 2001 inatamka “Kuwe na Sekta ya Mifugo ambayo ifikapo mwaka 2025 kwa sehemu kubwa, itakuwa na ufugaji wa kisasa na endelevu, yenye mifugo bora, yenye uzalishaji mzuri, inayoendeshwa kibiashara na yenye kuboresha lishe ya Mtanzania, kuinua kipato cha mfugaji na Taifa na kuhifadhi mazingira”.

Sera ya Taifa ya Uvuvi ya mwaka 1997 inalenga kuweka mazingira mazuri ya kuhifadhi na kuendeleza rasilimali za uvuvi. Tamko hili linalenga katika ukuzaji wa matumizi endelevu ya rasilimali za uvuvi ili kuongeza chakula, mapato, ajira na kuweka usimamizi madhubuti wa mazingira ya majini ili kudumisha maendeleo ya jamii.

2.0.  Majukumu ya Idara ya Mifugo na Uvuvi

Idara ya Mifugo na Uvuvi Halmashauri ya Mji wa Babati inatekeleza majukumu yake kwa wafugaji kama inavyoonesha hapa chini:-

i.    Kufanya uchunguzi wa magonjwa ya mifugo kwa wafugaji katika kata zote za Halmashauri.

ii.    Kukagua nyama na usafi wa machinjio mara kwa mara.

iii.    Kutibu magonjwa ya mifugo na kushauri wafugaji jinsi ya kukinga mifugo dhidi ya magonjwa.

iv.    Kutembelea wafugaji mara kwa mara na kuwapa ushauri fasaha wa kitaalam.

v.    Kukusanya takwimu zote za maendeleo ya mifugo katika eneo la Halmashauri.

vi.    Kufanya uhamilishaji (Artificial Insemination) na uzalishaji (breeding) wa mifugo kwa jumla.

vii.    Kushauri wafugaji kuhusu mbinu bora za kuzalisha maziwa na utunzaji wa ndama.

viii.    Kushauri wafugaji umuhimu wa kupunguza mifugo yao kulingana na maeneo/malisho.

ix.    Kutoa taarifa za milipuko ya magonjwa na viumbe waharibifu.

x.    Kuandaa ratiba cha chanjo na mipango ya uchanjaji

xi.    Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wakala wa pembejeo muhimu za mifugo.

xii.    Kuwa kiungo kati ya vikundi vya wafugaji na watafiti.

xiii.    Kukagua na kuidhinisha vibali vya usafirishaji wa mifugo.

xiv.    Kuendeleza uvunaji endelevu wa samaki na viumbe wengine wa baharini, maziwa, mito, mabwawa na malambo

xv.    Kutoa ushauri wa kitaalam kuhusu uvuvi bora, utengenezaji na uhifadhi bora wa samaki na mazao ya uvuvi, biashara na masoko ya samaki pamoja na ufugaji wa samaki na viumbe wengine wa majini

xvi.    Kutoa leseni za uvuvi na kuendesha mafunzo ya taaluma ya uvuvi

xvii.    Kusimamia na kutekeleza sheria za uvuvi (kwa mfano kuzuia uvuvi haramu)

xviii.    Kuratibu shughuli za utafiti wa uvuvi

xix.    Kutoa ushauri na mafunzo kwa wananchi juu ya uendelezaji na matumizi endelevu ya rasilimali ya uvuvi

xx.    Kukagua ubora wa samaki na mazao ya uvuvi na kuweka viwango vya kitaifa.


a)    Shughuli za kawaida.

•    Kukagua nyama

•    Kutoa kinga na tiba kwa mifugo

•    Kutoa elimu juu ya Ukaushaji wa ngozi

•    Uogeshaji wa mifugo

•    Kutoa huduma mbalimbali kama kukata kwato, kukata mikia, kuhasi, kukata midomo.

•    Kusimamia, kulinda na kuhifadhi rasilimali za ziwa Babati kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

•    Kudhibiti uvuvi haramu

•    Kutoa elimu ya uvuvi endelevu juu ya matumizi endelevu ya ziwa Babati

•    Kutoa elimu ya ufugaji wa samaki bwawani


b)    Miradi ya maendeleo.

•    Ukarabati wa machinjio ya Halmashauri ya Mji

•    Ujenzi wa ofisi ya uvuvi mtaa wa Nangara ziwani

•    Kufanya utafiti katika ziwa Babati

•    Kujenga uzio, choo na maji katika mnada wa Gendi


4.0. Hali ya watumishi

Idara ya Mifugo na Uvuvi inahitaji watumishi 18 ambapo kwa sasa wapo watumishi 14 hivyo kuwa na upungufu wa watumishi 4.


5.0. Vitendeakazi

Idara ya Mifugo na Uvuvi ina pikipiki 8 na kuwa na upungufu wa pikipiki 5, laptop 3 pungufu ni laptop 3, desktop mbovu 2 pungufu desktop 2, printer 1 pungufu 2.


6.0. Changamoto za idara

Ukosefu wa fedha kwa ajili ya kutekeleza shughuli za mifugo ikiwemo miradi, vitendea kazi, uvuvi haramu.


7.0. Utatuzi wa changamoto

Kuendelea kihimiza Halmashauri kutoa fedha za kutosha ili kuweza kutekeleza shughuli za idara.

Matangazo

  • Tangazo kwa waliopimiwa na kurasimishiwa viwanja - Sawe na Nangara December 25, 2022
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza - 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU November 09, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI NGAZI YA TATU July 27, 2022
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Miaka Miwili ya Rais Samia Manyara ni Shangwe tupu

    March 18, 2023
  • Waziri Kairuki atoa angalizo utekelezaji mradi wa BOOST

    December 13, 2022
  • Mhe. Jenista Mhagama awasisitiza watendaji wa ofisi yake kuwa na kauli nzuri na kutoa huduma bora kwa wananchi na watumishi wanaowahudumia

    December 04, 2022
  • Maagizo ya DC Twange kwa Watumishi wa Umma na Wafanyabiashara kuhusiana na utoaji wa risiti za EFD

    December 02, 2022
  • Tazama zaidi

Video

Halmashauri ya Mji wa Babati kuelekea miaka 61 ya Uhuru
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati